ReverbNation: MY MUSIC LIBRARY | MY MIXTAPES - LISTEN, BUY OR DOWNLOAD Here Now ;-)

Sunday, June 9, 2013

Orodha kamili ya washindi wa ‘Kili Music Awards 2013’

Jana ulikuwa usiku wa Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2013, ambapo ugawaji wa Tuzo hizo ulifanyika pale Mlimani City sambamba na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali. 

Waliofanya Vizuri kwenye Tuzo hizo ni Kala Jeremiah na Ommy Dimpoz ambao kila mmoja alijinyakulia Tuzo tatu. Hosts wa tuzo hizo walikuwa ni Zembwela na TJ. Angalia list nzima ya tuzo hizo hapa:

Friday, June 7, 2013

Picha: Hatimaye Mar. Albert Mangweha aka Ngwair jana amezikwa kwenye makaburi ya Kihonda, Morogoro

Hatimaye Mar. Albert Mangweha aka Ngwair jana amezikwa kwenye makaburi ya Kihonda mkoani Morogoro ambako ni nyumbani kwao. 

Hapa ndipo alipolala Ngwair. Kabla ya kuzikwa, wananchi wa Morogoro walipata fursa ya kuuaga mwili wake kwenye uwanja wa Jamhuri. RIP Ngwair!!!

Monday, June 3, 2013

Confirmed: Show ya ‘Miaka 13 ya Lady Jaydee’ kufanyika tarehe hii...

Hatimaye mwanadada mkongwe wa muziki wa kizazi kipya, Lady Jaydee ameweka wazi tarehe ya Show yake ya kuadhimisha miaka 13 kwenye muziki na uzinduzi wa album yake mpya ya Nothing but the truth.

Kupitia mtandao wa Twitter jana, Lady Jaydee aliitangaza tarehe rasmi ya Show hiyo ambapo #TeamAnaconda wameonesha kufurahia taarifa hiyo. Jide kupitia mtandao huo ameandika:

Upcoming Event: Charismatic Bash @ Mbalamwezi Beach - Mikocheni

Event: Charismatic Bash.
Venue: Mbalamwezi Beach - Mikocheni.
Date: 29.06.2013.
Entrance: 5,000/=
Tickets: Steers - Makumbusho, Puma Petrol Station - Mwenge.

Kutakuwa na Exclusive Performance kutoka kwa Swish na wasanii wengine wakali, usiikoseeee!!! “Lets meet where the fun is, teens!

Big Brother Africa: Huddah (Kenya) na Denzel (Uganda) waaga mashindano, kura zao hazikutosha

Kwenye shindano la 8 la Big Brother Africa (The Chase), mambo yameanza sasa. Tumeshuhudia mambo kadhaa yaliyokua yanafanyika ndani ya jumba hilo ambayo yametufanya tuendelee kufatilia kwa ukaribu.

Jana ilikua siku ya kuondoka kwa washiriki wawili ambao walipata kura chache baada ya kuwa kwenye danger zone. Uganda's Denzel and Kenya's Huddah wamekuwa wa kwanza kuyaaga mashindano hayo.

Sunday, June 2, 2013

Wema Sepetu: ‘Toka nimeanza mapenzi na Naseeb (Diamond) sikuwahi kum-cheat’

Source: Tanzania Movies.
“Maisha yangu yote toka nimeanza mapenzi na Naseeb naweza kusema kuwa sikuwahi kuwa unfaithful. I used to be very faithful to him na tulikuwa tunapendana sana. With Naseeb (Diamond Platnumz) nilikuwa nimesharidhika na maisha ambayo niko nayo”

Hayo si maneno yetu bali ni maneno aliyoyasema mwanadada Wema Sepetu katika mahojiano yake na jarida ya Mzuka.

Picha: Mtoto wa Rais Kikwete, Miraji Kikwete ametoa vazi rasmi la kumuenzi Ngwair

Mtoto wa Rais Kikwete, Miraji Kikwete ametoa vazi rasmi la kumuenzi Ngwair. Rest in Peace Cow Boy (Ngwair)!!!